PAROKIA YA LUHANGA


MAMBO YA JUMLA YA PAROKIA

Jina la parokia ni mtakatifu yohane mbatizaji luhanga
-Msimamizi wa parokia ni mtakatifu yohane mbatizaji
- Jina halifanani na parokia nyingine za jimbo la Dar es salaam

Mahali parokia ilipo ni Wilaya ya Ubungo kata ya Mabibo Farasi.

Parokia ilitangazwa rasmi 20 january 2013

Parokia ipo katika dekania ya Ubungo

Idadi ya waumini katika parokia Mpaka kufikia 2016 ilikua ni kati ya waumini 7500 na imepatikana kwa njia ya sense iliyofanyika 2016 kwa waumini kujaza fomu maalumu.kwa sasa kuna waumini Zaidi ya 7500.Sensa nyingine inatarajiwa kufanyika 2018

Jumuiya zilikuwa (25) lakini kutokana na watu wengi kuhamia jumuiya hizo zimefikia 47.

Parokia ina kigango kimoja kinachofahamika kwa jina la mt Peter Feba. Na kipo Mabibo na kina kanda,Jumuiya 16.

Parokia ina idadi ya jumuiya 65 na zinatumia majina ya watakatifu.

Kila jumuiya ina kaya kati ya 20-25

Jumuiya zinasali mara moja kila siku ya jumamosi kuanzia saa 12:30 kwa kufuata mwongozo wa jumuiya ndogo ndogo toka Jimboni

Kanda husali mara moja kila baada ya mwezi mmoja mwisho wa mwezi.

Maudhuri kwa jumla katika JNNK ni ya wastani, na maudhurio huwekwa katika kumbukumbu.

Viongozi wa kamati tendaji wana utaratibu wa kuzitembelea jumuiya JNNK , Kanda na pia misa zinasomwa.

Kanda JNNK hua zinaadhimisha Misa takatifu za somo wa jumuiya na kanda kwa kuomba kibali kutoka hierakia.

Uongozi wa jumuiya umekamilika na pale ambapo inapotokea kuna mapungufu yanajazwa mara moja kwa kuitisha uchaguzi mdogo.

Uongozi wa Halmashauri ya walei parokia hukutana kila baada ya miezi miwili, na kwa kanda ni baada ya miezi mitatu.

Huduma za kiroho na jamii hutolewa katika JNNK/Kanda na mitaa kama ifuatavyo.
a) Misa za somo wa jumuiya
b) Huduma za kutembelea wagonjwa na kuwapa sacrament
c) Ujazaji fomu kwaajili ya maombi ya sakramenti kama Ubatizo, Komunio ,kipaimara, na huduma zingine zitolewazo na kanisa.
d) Kutembelea waumini na kuhimiza juu ya kufanyika sacrament mbalimbali pamoja na kuhimiza kuondokana na uchumba sugu.

Changa moto kubwa zilizopo ni maudhurio madogo kwa waumini kwenye Jumuiya , Mikutano,na hata semina.

Pia kuna mwamko mdogo katika utoaji michango inayohusu kanisa

Changamoto nyingine ni michango kuwa mingi kanisani.

UONGOZI
Kamati tendaji ipo na imekamilika kikatiba

Kamati tendaji ya parokia hukutana mara moja kila mwezi siku za jumamosi na kikao kinachukua muda wa masaa mawili kujadili .Baba paroko ni mshiriki katika kikao hicho.

Vikao vya dharura hufanyika pale vinapo hitajika.

Halmashauri ya walei ya parokia inaundwa na viongozi watano wa kila jumuiya pamoja na wenyeviti wa vyama vya kitume na inakutana mara moja kila baada ya miezi mitatu.

Agenda na taarifa za vikao zinapatikana kwa wakati na zinatunzwa.

Parokia haijawa na ofisi za halmashauri ya walei ya parokia, lakini mipango ipo ya kuwa na ofisi na vitendea kazi vya ofisi vipo baadhi, lakini computer inatumika ni ya ofisi ya paroko.

Njia za mawasiliano kwa wajumbe wa kamati tendaji pamoja na halmashauri ya walei ni :

Kwa njia ya barua pepe(yaani E mail) simu,Whats aap, lakini zaidi ya hapo ni kwa matangazo kanisani.

Anuani ya barua pepe yaani E mail ya parokia ipo.

Zipo kamati ndogo ndogo za kikatiba na zimekamilika,

kamati hizo hua zinakutana mara mara.

Zipo kamati zingine Ambazo sio za kikatiba na zinaripoti kwa kamati tendaji ya parokia, kamati hizi ni kama zifuatazo:
a) Kamati ya ujenzi
b) Kamati ya uhamasishaji.

Kamati zote za kikatiba na zisizo za kikatiba zinaripoti kwa kamati tendaji ya paarokia

kamati hizi hazina mwingiliano lakini kuna wakati zinashirikiana

Dira malengo na mikakati ya parokia

  • DIra ; Dira ya Parokia ni kuwajenga waumini kiroho hasa wale wwanaoonyesha kukata tamaa ikiwa ni pamoja na kuwatembelea
  • Malengo;Kuendeleza mipango ya parokia kama ujenzi wa kanisa la kudumu la kigango cha MT Peter Feba kilichopo mabibo na kumaliza jingo la vijana.
  • Mikakati ya parokia; Mikakati ya parokia inaendana na utekelezaji wa malengo ya mikutano halmashauri ya walei itakapo pangwa na parokia.

Ipo kalenda ya matukio ya mwaka ya kiparokia amabayo imetengenezwa kwa ushirikishwaji wauminiWaamini wanaarifiwa mipango ya parokia kwa kupitia maatangazo kanisani , pia kupitia JNNK kupita halmashauri ya walei ya parokia au viongozi kutembelea jumuiya na kueleza jambo husika.

VYAMA MASHIRIKA NA JUMUIYA ZA KITUME (VMJ)

Vipo vyama vya kitume 13na vikundi 3

Vyama hivi vina wachama wa wastani vinakidhi mahitaji ya parokia

Vyama na vikundi vya kitume vinafanya kazi kulingana na katiba ya halmashauri ya walei ya jimbo.na vyama vyote hivi viko hai

Vyama hivi havina ofisi parokiani, lakini vinalelewa na vipo chini ya paroko.

Wasimamizi wake wamegawanyika katika makundi, yaani Makatekista, Masista na kamati tendaji ya parokia.

VMJ vinatoa taarifa na repoti pamoja na ya fedha mara kwa mara kwa uongozi wa parokia

Na pia vinajitegemea na viko chini ya uangalizi wa parokia

Vyama vina ushirikiano mzuri katika dekania na katika ngazi ya jimbo

VMJ haina mambo maaalumu ambayo yanaweza kuigwa na parokia nyingine yote ni ya kawaida sana. Kama vile kuuza maadili katika jamii has kwa vijana.

SEMINA MBALIMBALI KATIKA UENDELEVU WA IMANI, UONGOZI NA UTEGEMEZAJI
Ziko semina ambazo zimeshafanyika kuanzia ngazi ya JNNK, VMJ na hadi Parokia

Mafungo na semina mbalimbali ziinaendelea kuandaliwa kutokana na ratiba ya parokia.

Vyama vya kituume vina ongozwa na ratiba yake maalumu.

Viongozi wa kamati tendaji wamefanyiwa semina .

Semina za kiroho zinafanyika kwa kalenda ya parokia

Hali ya Imani kwa ujumla inaridhisha, na inatakiwa kuendelezwa kwa nguvu, lakini katika kipindi cha huruma ya Mungu Viongozi na hiarakia wameweza kuhamasisha waumini waliokuwa na ndoa , Ndoa thelathini na tano zimeweza kufanikishwa.

Kimsingi hali ya utoaji parokiani ni ya wastani na kiasi inaridhisha.

Hali kadhalika utoaji wa zaka kama amri ya kanisa upo kwa kiwango cha chini.

Parikia inatoa michango ya jimbo kamili kama inavyo paswa

FEDHA NA MIPANGO
Mpango wa fedha unaotumika ni ule wa jimbo

Mapato na matumizi ya parokia yanajulikana kwa waumini na yanatolewa taarifa.

Matoleo ya kila dominika yanatangazwa kwa waumini kila dominika inayofuata na kubandikwa kwenye mbao za matangazo ya kanisa.

Fedha zote zinazokusanywa hupelekwa benki kwa wakati

ULINZI NA USALAMA
Hali ya ulinzi na usalama parokiani ni ya kuridhisha, na ulinzi unafanywa na kampuni binafsi

MAENDELEO YA KIUCHUMI
Parokia ina miradi miwili
Shule ya chekechea
Na shule ya sekondari ya miaka miwili yaani Qt

Kwa sasa Parokia ipo katika ujenzi wa kigango cha Mt Peter Feba mabibo na jengo la vijana la parokia , na hali ni nzuri na waumini wanahamasishwa kuendelea kutoa michango yao.

Lakini pia ipo mipango ya kuwaendeleza waumini kiuchumi
a) Ipo saccos ya parokia waumini wanahamasishwa wajiunge
b) Mpango mwingine ni jingo la vijana na watoto wa utoto mt
c) Malengo mengine ni kuwa na vyarahani ili kuwaendeleza vijana

MAMBO YA JUMLA
Parokiia haina mgogoro wowote wa kimipaka

Kwa sasa parokia haina mipango yeyote ya kuwaendeleza waumini wake kiuchumi isipokuwa kwa kadiri parokia inavyokuwa itafanya juu chini mipango hiyo iwepo

Idadi ya mapadre inatosheleza

Parokia ina wanasemiri 11 kwa ujumla katika seminari mbalimbali

Hakuna waumini waliojiunga na utawa katika parokia yetu

Maandiko kuhusu historia ya parokia picha waamini na picha za miradi zipo baadhi na zinaaendelea kufanyiwa kazi.

Mwisho tunawashukuru kwa ushirikiano wenu.

JE UNATAFUTA

PAROKIA?

Upate majibu yako haraka zaidi
Ramani ya Parokia
Hakuna ramani kwa sasa...
Kuhusu Kanisa Katoliki

Ofisi ya Halmashauri ya Walei Jimbo Kuu la Dar es salaam inapatikana makao makuu ya Jimbo,
Kanisa la St. Joseph, barabara ya Sokoine na Manseld street.

P.O Box 167, Dar es Salaam, Tanzania
Tel: +255 762 024 199
Email: mawasiliano@waleijimbodaresalaam.org
            darwaleijimbo@yahoo.com
Web: www.waleijimbodaresalaam.org

Kwa Habari kemkem za Kanisa jiunge nasi

Andika email yako hapo juu, na upokee taarifa za H/walei

Copyright © 2025. All Rights reserved by H/Walei Jimbo Kuu la Dar es salaam