DEKANIA YA ST.JOSEPH
DEKANIA YA UBUNGO
VIONGOZI WA DEKANIA YA KIBAHA
DEKANIA PETERS
DEKANIA YA ST. GASPAR
DEKANIA YA UKONGA
DEKANIA YA SEGEREA
DEKANIA YA KIGAMBONI
DEKANIA YA KILIMAHEWA
PAROKIA YA MT AMBROSE TAGASTE
n/a
A:MAMBO YA JUMLA YA PAROKIA
Jina la parokia Mt ambrose na haliingiliani na parokia nyingine za jimbo
Kijiografia
Parokia inapatikana katika mtaa wa kimara B kata ya saranga
Kaskazini-bikira maria mama wa huruma
Kusini-Temboni St Augustino
Mashariki-Bikira maria mkingiwa dhambi ya asili mavurunza
Magharibi-Teresia motto yesu mbezi
Parokia hii inapatikana katika Dekania ya Mt Monika Kibaha
Parokia inawaumini wapatao 3457 hii ni kwa mujibu wa sense ya waumini iliyofanyika feb 2017
Sensa ya mara ya mwisho inatarajiwa kufanyika tena 2019
Parokia ya mt Ambrose ina kigango kimoja ambacho ni Mt Monika Matosa.
Parokia inajumla ya kanda nne ambazo zimegawanyika kulingana na mipaka ya barabara.
kila kanda inawastani wa jumuiya (5).
Uongozi katika kanda umetokana na katiba ya halmashauri ya walei jimbo
Kanda nane zimepata majina ya watakatifu
Zipo pia jumuiya ndogo ndogo 40 na jumuiya zote zinatumia majina ya watakatifu
Kila jumuiya ina wastani wa kaya 15-20 na zinaonyesha kufanya vyema hazihitaji maboresho
Jumuiya za kikanda zinasali mara moja kwa mwezi kwa jumamosi ya mwisho ya mwezi, na muda ni saa 12:30 asubuhi.
Mwongozo unaotumika ni ule wa sala za jumuiya za asubuhi.
Maudhurio kwa jumuiya yanaridhisha lakini kwa kanda hayaridhishi. Wawumini wanahitaji kuhamasishwa zaidi
Kamati tendaji ya parokia inawajibika kuzitembelea jumuiya za kanda zao.
Jumuiya hufanya maadhimisho ya misa kwaajili ya mtakatifu wa somo wa somo wa jumuiya husika.
Uongozi katika jumuiya na kanda umekamilika bila mapungufu.
Uongozi wa halmashauri za jumuiya na kanda hukutana kila baada ya miezi mitatu.
Huduma za kiroho na kuombea wagonjwa hufanyika kila alhamisi kwa kutembelea waumini ikiwa ni pamoja na kutoa mpako wa wagonjwa.
Zipo kanda nane (8) nazo ni Mt Monika matosa, Mt monika namanga,, Mt ambrose, mt Anna, kanda ya mbezi matosa, Mt clara, Mt caroli luhanga
B:UONGOZI
Kamati tendaji ya parokia ipo na imekamilika
Kamati tendaji hukutana mara moja kila mwezi siku ya jumapili baada ya misa ya kwanza baba paroko na msaidizi wake wakiwepo.
Halmashauri ya walei parokia huundwa na
a. kamati tendaji ya parokia,
b. viongozi watano kutoka kila jumuiya ,
c. Kamati tendanji ya kigango ,
d. wenyeviti kutoka vyama vya kitume ngazi ya parokia pamoja na
e. wenyeviti wa ujenzi parokia na kigango
Jumla ya wajumbe wanokutana ni 34 wnaokutana mara nne kwa mwaka.
Ajenda za vikao husika hupatikana kwa wakati na kutunzwa
Halmashauri ya walei parokia kwa sasa haina ofisi hali kadhalika vitendea kazi.
Mawasiliano kati ya kamati tendaji na wajumbe hufanyika kwa njia ya simu na mitandao ya kijamii kama vile Whatsaa groups, Barua pepe yaani E mail, na njia nyingine ni matangazo yanayotolewa kanisani.
Kamati ndondogo za kikatiba zipo na zimekamilika
Kamati zisizo za kikatiba zipo na hukutana mara kawa mara, kamati hizo ni ;
-Kamati ya ujenzi,
-Kamati ya ardhi na - kamati ya ulinzi na usalama.
Kamati zinafanya kazi kwa mujibu wa katiba
Kamati zote za kikatiba na zisizo za kikatiba zinaripoti kwa kamati tendaji ya parokia
Kamati hizi zinafanya kazi kwa umakinifu na mawasiliano lakini hakuna maingiliano katika utendaji
Dira mikakati malengo ya parokia vipo kupitia kamati ya fedha na mipango na maazimio ya utekelezaji yanapitishwa na mikutano ya halmashauri ya walei parokia.
Kalenda ya matukio ya kiparokia ipo
Njia zinazotumika kuwaarifu waumini kuhusu mipango ya paarokia ni kwa kupitia :
a. Matangazo ya siku za dominika
b. Mikutano ya halmashauri ya walei ya parokia.
c. Viongozi kuongea na waumini kanisa
d. Viongozi kutembelea jumuiya na kueleza jamabo husika.
Vyama mashirika na jumuiya za kitume (VMJ)
Vyama mashirika na jumuiya za kitume vipo na vina fanya kazi zake za kitume kama kawaida, vyama hivi vipo 11
-wawata,uwaka,Utoto mtakatifu,Regio maria, Viwawa. Na watumishi wa altare
Baadhi ya vyama hivu havina wanachama wa kutosha , lakini baadhi vina wanachama wa kutosha ,Wastaafu,moyo mt wa yesu, Karismatiki, St vicent, mt Rita.
Vyama vya vikundi hivi vya kitume hufanya kazi kulingana na katiba ya halmashauri ya walei na kutimiza wito wa kitume
Uhai wa vyama hivi ni wa wastani
VMJ havina ofisi kwa sasa parokiani wala vifaa kuwwezza kukidhi mahitaji katika kufanya shughuli zake za kiofisi.
Vyama hivi hulelewa na paroko ambaye ndiye mlezi kwa sasa
VMJ hutoa taarifa au ripoti (pamaoja nay a fedha) mara kwa mara katika uongozi wa kamati tendaji
Ushirikiano na ushiriki wa VMJ katika shughuli za kidekania na jimbo uko vizuri.
SEMINA MBALIMBALI KATIKA UENDELEZI WA IMANI UONGOZI NA UTEGEMEZAJI
Ziko semina za kijumuiya ambazo zimesha fanyika,lakini pia kwa sasa zipo semina nyingine ambazo zinzandaliwa parokia zifanyike.
Kamati tendaji ya parokia ilisha patiwa semina ya uongozi
Hali ya Imani kwwa sasa ni nzuri lakini baado juhudi Zaidi zinahitajika ili kuimarisha ustawi wa kiimani.
Swala la utoaji si zuri sana lakini lina ridhisha kwa kiasi Fulani.
Utoaji zaka kama amri ya kanisa una suasua
Parokia inatoa michango kwajimbo kikamilifu na kwa wakati jinsi inavyo paswa.
FEDHA NA MIPANGO
Parokia inatumia mpango wa fedha wa jimbo
Parokia huwajulisha waumini mapato na matumizi kwa kuwasomea taarifa ya fedha mara nne kwa mwaka.
Matoleo ya kila dominika hutangazwa kwa waumini kila dominika inayofuata
Fedha za parokia hupelekwa benki kwa wakati
ULINZI NA USALAMA.
Hali ya ulinzi na usalama katika parokia ni nzuri.
Walinzi wanaotumika ni kutoka kampuni binafsi.
MAENDELEO YA KIUCHUMI
Hakuna shughuli za miradi.
Kwa sasa kuna maendeleo ya ujenzi wa nyumba ya mapadre na kanisa la kudumu kigangoni.
MAMBO YA JUMLA
Parokia kwa sasa haina migogoro ya mipaka yake.
Kwa sasa parokia haina mpango makhususi wa kuwaendeleza waumini wake kiuchumi isipokuwa kadiri parokia inavyoendelea kukua itafanya juu chini mipango hiyo iwepo.
Idadi ya mapaadre /watawa haitoshelezi.
Ipo historia ya parokia pale itakapo hitajika.