PAROKIA YA MTONI TEMEKE


Somo wa parokia ni Josephine Bakita

Parokia ilizaliwa  1996

Kijiografia parokia inapatikana maeneo ya mtoni kwa azizi ali. wilaya ya temeke

uongozi
Parokia ipo chini ya paroko Fr Anthony Mashaka akishirikia na Fr Emmanueli Morweng wote wa shhirika la Stigmatine (madonda matano ya kristo)

Parokia ina jumla ya jumuiya ndogo ndogo 34 ambaazo zimo ndani ya kanda 12.

Viongozi wake wamechaguliwa kwa mujibu wa katiba ya Halimashuri ya Walei

Sala za jumuiya ni kwa mujibu wa mwongozo wa sala za jumuiya.

Maazimio ya parokia

Maazimio ya parokia yamejikita katika Nyanja mbili
a)    Ya kiroho
b)    Ya kijamii,kiuchumi na maendeleo ya parokia
   
Ya kiroho
•    Kuwa na semina mbalimbali, ubatizo wa watoto waliozaliwa nje ya ndoa, kuwa na ndoa za pamoja ,hivyo waliobatizwa kwwanzia 2016 hadi desember ni 126 wakatekumeni 20, komunio ya kwanza 82, kipaimara66 na waliofunga ndoa 25
•    Vyama vya kitume kuratibu kuabudu ekarist takatifu kila alhamisi
•    Kualika wahamasishaji wa ndani nan je ya parokia  kuhamasisha kanisani .
•    Kamati tendaji kuwa na ziara za kikanda
•    Kufanya semina mbalimbali za makundi ya kitume (UWAKA, WAWAATA ,SHIKWAKA n.k
•    Mafungo semina na hija, katika kipindi cha mwaka 2016 ka mfano zimeendeshwa semina mbalimbali za mafungo ukizingati ilikua ni mwaka wa huruma.
Semina mbalimbali zimesaidia kuwaimarisha waumini kiroho kwa mfano
Visiga WAWATA na Hija Pugu UWAKA, Novena kwa wanaparokia wote

•    Katika kuwakuza waumini kiroho,  parokia imewaandaa maketekista wawili kwa kushirikiana na mapadre katika kufanya shughuli za kiroho  ikiwa kuwaandaa vijana katika mafundisho mbalimbali ya kiroho kama vile ubatizo wa wa katukomeni, komunio na hata kipaimara.
   
Ya kijamii , kiuchumi na kimaaaendele ya parokia
Chanzo cha mapato ya paroki kinatokana sana na:
         - Sadaka za kila dominika
         - Mavuno
         - Shukrani

Maendeleo  ni pamoja na ujenzi wa kanisa, lakini pia kijamii ina tengeneza mashirikiano.

Vyama /mashirika ya kitume na vikundi

Vyama hivyo ni kama vifuatavyo:
a)    UWAKA
b)    WAWATA
c)    Shirika la mt Augustino la wazee na wastaafu
d)    Moyo mt yesu
e)    Legio maria
f)    Karismatiki katoliki
g)    SHIKWAKA
h)    Utoto mtakatifu
i)    Umoja wa vijana(VIWAWA)
j)    Shirika la mt Fransis wa azizi (VIAFRA)
k)    Wajane na Wagane
l)    Wasoma masomo altareni

Ili kuleta umoja  wa vyama vyote vya kitume parokiani , limeanzisha shirikisho la vyama vya kitume (SHIVYAKI) pamoja na uongozi wake

Mwongozo shughuki za kamati tendaji na halmashauri ya walei

Shughuli zote za Halmashauri ya walei huongozwa na katiba ya halimashauri ya walei katoliki Tanzania TEC) ya mwaka 2013 pamoja na maagizo ya babab paroko. Kamaati tendaji pia huratibu shughuli za jimbo na matukio mbalimbali

Kamati mbalimbali

Kuna kamati mabalimbali ambazo zimeundwa katika kusaidia mafanikio ya parokia katika utume nazo ni :

Kamaati ya malezi na familia
Kazi yake kuratibu changamoto zoto zinazohusiana na malezi na familia ; mfano mzuri ni swala la ndoa na familia,

Kamaati ya liturjia
Kamati hii kazi yake ni kutoa mwongozo wa kiliturjia

Kamati ya haki na Amani
kuwaelimisha waumini kuzijua haki zao mbalimbali za kuchagua na kuchaguliwa katika maswala mbalimbali ya kijamii, Pia kuijua na kuisimamia katiba ya walei n.k

Kamati ya mafundisho ya elimu na dini

JE UNATAFUTA

PAROKIA?

Upate majibu yako haraka zaidi
Ramani ya Parokia
Hakuna ramani kwa sasa...
Kuhusu Kanisa Katoliki

Ofisi ya Halmashauri ya Walei Jimbo Kuu la Dar es salaam inapatikana makao makuu ya Jimbo,
Kanisa la St. Joseph, barabara ya Sokoine na Manseld street.

P.O Box 167, Dar es Salaam, Tanzania
Tel: +255 762 024 199
Email: mawasiliano@waleijimbodaresalaam.org
            darwaleijimbo@yahoo.com
Web: www.waleijimbodaresalaam.org

Kwa Habari kemkem za Kanisa jiunge nasi

Andika email yako hapo juu, na upokee taarifa za H/walei

Copyright © 2025. All Rights reserved by H/Walei Jimbo Kuu la Dar es salaam