PAROKIA YA VIKINDU


KANISA KATOLIKI LA MT. VINSENT WA PAULO – VIKINDU

HISTORIA:
Inaelezwa kuwa Parokia ya Vikindu ilianza mwaka 1960 kama Jumuiya chini ya Parokia ya Mbagala Mission ikiongozwa na mkristu mmoja aliyeitwa kwa jina *Katekista Joseph Namiva (alifariki Augost 2008 na kuzikwa makaburi ya kanisa - Mmakonde kwa Kabila) ambaye akitokea Zanzibar. Mwaka 1980 muumini mmoja Capt. Joseph Mtahangarwa alitoa eneo lake la ekari 10 kwa kanisa ili kuwezesha kuwa eneo kubwa na kupata hadhi ya kuwa Kigango.

Wakati huo pale Parokiani Mbagala Mission*Pd. JOSEPH Bill (alifariki na amezikwa katika kanisa la BIKIRA MARIA Entebe –Uganda) wa shirika la Mt. Vinsent wa Paulo lenye asili yake Kerela (India) alikuja kutokea Kigoma (Tanzania) mara kwa mara kwaajili ya mafungo.


Miongoni mwa walioshiriki alikuwa Ndugu Joseph Mtahangarwa ambaye alikuwa akiishi jirani na kanisa dogo la kigango hiki. Baada ya maafungo hayo alimkaribisha Pd. Bill nyumbani na kumkabidhi sehemu ya eneo lake la ekari 8 kama shukrani kwa Mungu lakini pia kukaribisha huduma hii ya mafungo katika eneo la Vikindu (Soweto).
“Jina SOWETO lina asili ya mji wa SOWETO huko Afrika ya Kusini ambapo yalitokea mauaji ya waafrika wengi kwa sababu ya ubaguzi wa rangi (SOWETO MASACRE 1976) hivyo katika mji huu kulikuwa na mauaji ya watu kwa sababu eneo hili kulikuwa na mapori mengi, hata baada ya kujengwa barabara ya rami kulikuwa na ajali nyingi zikitokea mara kwa mara hivyo kuakisi jina SOWETO kwa maana ya mauaji” (Mzee Husein Jackson)

Historia inaonesha mwaka 1997, Mapadre wa shirika (Pd. JAMES) kutoka Kerela (India) waliingia Soweto-Vikindu na kuanza kazi ya kichungaji pamoja na kununua eneo jingine ili kuongezea. Wakati wananunua maeneo kwa wenyeji; wenyeji wengi waliwauliza mapadre;
“maeneo haya mnayonunua ni kwaajili gani? nao walijibu “tunataka kuufanya huu mji kuwa mji wa YESU (JESUS TOWN)” tokea hapo mji huu ulitambulika kama mji wa Yesu ingawa siku hizi za jirani jina hili limekuwa likififia”


Kanisa dogo la Kigango lililojengwa kwa miti na udongo na kuezekwa kwa bati liliendelea kuchoka hali ambayo ilipelekea baadhi ya bati kuanza kuvuja. Katekista wa kwanza kigangoni hapa Ndugu *Joseph Namiva aliendelea kutoa huduma ya kiroho kigangoni na ujio wa mapadre hawa wa shirika la Mt. Vinsent wa Paulo uliongeza chachu ya huduma ya kiroho katika mji wa Yesu.
(Picha zinapatikana katika albam iliyopo ofisi ya Baba Paroko)

Miaka ya 1980 Kigango hiki kilihamishwa toka Mbagala Mission kuja Parokia ya Mt. Xavery Mkuranga. Paroko wa wakati huo wa Parokia ya Mkuranga Pd. Patrick akisaidiana na Mapadre wa Mt. Vinsent wa Paulo waliendelea kuhudumu kanisa na kuendeleza uinjilishaji katika Kigango hiki cha Vikindu.

Mwaka 1999 ujenzi wa kanisa dogo katika nyumba ya Mapadre wa Mt. Vinsent ukawa umekamilika; kwa kuwa kanisa la Kigango lilikuwa linavuja na baaadhi ya kuta kuwa zimeharibika; Pd. JAMES aliwaomba waumini wa Kigango hiki wasali katika kanisa lililoko nyumba za mapadre badala ya kanisa la kigango ambalo lilikuwa limeharibika.

Wakati huo kanisa lilikuwa na jumuiya 2 na waumini waiopungua 100 na wasiozidi 200
Kigango hiki kilipata kuwa Parokia mwaka 21/01/2001 uzinduzi huo ulifanyika Mwadhama Polycap Kadinali Pengo na kukabidhiwa kwa shirika la Mt. Vinsent wa Paulo. bila jengo la kudumu la kanisa, wakati huo Parokia ilikuwa na vigango 7.
(Picha zinapatikana katika albam iliyopo ofisi ya Baba Paroko)

Waumini walisali kwa muda katika kanisa dogo lililopo nyumba kwa mapadre kisha Pd. James alisema
“waumini hawa wakiendelea kusali katika kanisa hili hawatajenga
kanisa la parokia”
maamuzi haya yalipelekea waumini kujenga hema katika eneo la kanisa wakati huo eneo la kanisa liliko kando ya barabara ya kilwa badala ya lile la zamani ambalo kanisa lilibadilishana na shirika la masista wa Bikira Maria Mama wa Mlima Carmel. Siku moja wakati wa maandalizi ya ibada katika hema hilo ukaja upepo mkali uliopeperusha maandalizi yote ya ibada, wakati huo Paroko Pd. James alikwenda likizo India, ndipo Pd Joseph akasema
“na turudi tukasali katika kanisa dogo nyumbani kwa mapadre mpaka ujenzi wa kanisa la parokia utakapo kamilika”.
jiwe la msingi la ujenzi wa kanisa la Parokia liliwekwa na mwadhama Polycapy Kadinali Pengo tarehe 27/09/2002. Kanisa hili la parokia lilitabarukiwa na Mwadhama Polycapy Kadinali Pengo Askofu Mkuu wa jimbo kuu la Dar es salaam tar. 24/09/2006
(Picha zinapatikana katika albam iliyopo ofisi ya Baba Paroko)

Pamoja na Mapadre hawa baadae mwaka 2000 Shirika la masista wa Huruma ya Mungu wa Mt. Vinsent wa Paulo kutoka Austria walikuja hapa Vikindu, walijenga makazi yao, zahanati na shule ya watoto wadogo (chekechea).
Tena Mwaka 2001 shirika lingine la masista wa Bikira Maria Mama wa Mlima Carmel kutoka Kerela India walikuja katika Parokia ya Vikindu kwa sasa wamekwisha kujenga nyumba ya Malezi pamoja na shule ya msingi na sekondari

Hadi leo Parokia ina jumla ya vigango 7 kanda 9 jumuiya 74 na waumini wapatao 3,984

Huduma ya mafungo kama ilivyo kusudiwa tokea awali rasmi ilianzishwa mwaka 2015 na aliyekuwa Paroko mwaka huo Pd. Steven Shaiju na inaendelea Parokiani ingawaje ujenzi wa kituo rasmi cha mafungo uko katika mpango wa vingozi wa mapadre wa shirika la Mt. Vinsent wa Paulo.


MAPAROKO WALIOKWISHA HUDUMA KATIKA PAROKIA HII
1. Pd. JOSEPH
2. Pd. JAMES
3. Pd. JINNU
4. Pd. TOMMY
5. Pd. MATAYO
6. Pd. SHAIJU
7. Pd. JINSO

MAPADRE WALIOKWISHA HUDUMU KATIKA PAROKIA HII KWA JUMLA
1. Pd. BILL
2. Pd. JAMES
3. Pd. PAUL
4. Pd. JOSEPH (MANDEVU)
5. Pd. JOSEPH
6. Pd. JOY
7. Pd. JINNU
8. Pd. TOMMY
9. Pd. MATAYO
10. Pd. BIJU
11. Pd. JIBIN
12. Pd. IBIN
13. Pd. JINSO
14. Pd. JACOB
VIONGOZI WALEI WALIOKWISHA KUHUDUMU PAROKIA (wanaokumbukwa


NO.
JINA
CHEO
MIAKA
1.
CHRISTIAN MUSHI
MWENYEKITI
2001- 2010
2.
PIUS MGAYA (2016)
KATIBU

3.
FAUSTIN ONYANGO
MWENYEKITI
2010 - 2013
4.
SIXMUND FUSSY
KATIBU

5.
MARTINA MSONGO
K/MSAIDIZI

6.
ANNA CHARLES MWAMBUSI
MHAZINI

7.
ERICK MWAMBELEKO
MWENYEKITI
2013 -
8.
MAKARIOUS KIHAWA
M/MWENYEKITI

9.
ANGRIBETH NKWERA
KATIBU

10.
SIRILY MALLYA
M/KATIBU

11.
MONIKA GODFREY
MWEKAHAZINA


JE UNATAFUTA

PAROKIA?

Upate majibu yako haraka zaidi
Ramani ya Parokia
Hakuna ramani kwa sasa...
Kuhusu Kanisa Katoliki

Ofisi ya Halmashauri ya Walei Jimbo Kuu la Dar es salaam inapatikana makao makuu ya Jimbo,
Kanisa la St. Joseph, barabara ya Sokoine na Manseld street.

P.O Box 167, Dar es Salaam, Tanzania
Tel: +255 762 024 199
Email: mawasiliano@waleijimbodaresalaam.org
            darwaleijimbo@yahoo.com
Web: www.waleijimbodaresalaam.org

Kwa Habari kemkem za Kanisa jiunge nasi

Andika email yako hapo juu, na upokee taarifa za H/walei

Copyright © 2025. All Rights reserved by H/Walei Jimbo Kuu la Dar es salaam