PAROKIA YA KURASINI


Jina la Parokia ni Parokia ya Kurasini , msimamizi wake ni Mt Maurusi.

Parokia ilizaliwa 1970

Parokia ya mtakatifu Maurus kijiogrfia ipo kurasini, Wilaya ya Temeke mkoa wa Dar es salaam

Parokia ipo katika dekania ya mtakatifu Joseph jimbo kuu la dar es salaam.

Parokia kwa mujibu wa sensa 2016 ni waumini wapatao 3450,

Kwa ujumla parokia haina vigango

Parokia ya Mt Maurusi ina kanda saba(7)

Katika parokia ya Mt Maurus kuna jumuiya zipatazo 46 na jumuiya zote zinatumia majina ya watakatifu

Kila jumuiya ina wastani wa kaya 15 kutokana na maelekezo. hapahitajiki maboresho yeyote kwa sasa.

Jumuiya ndogondogo nyingi zinasali siku ya jumamosi

Katika Parokia ya Mt Maurus viongozi wa kamati tendaji ndio wanotembele jumuiya na kanda. Mapadre wanatembelea familia moja moja

Katika Parokia jumuiya zina utaratibu wa kuadhimisha sherehe wa somo wa jumuiya na kanda.

Viongozi wote wanachaguliwa kwa mujibu wa katiba . Pale panapotokea mapungufu ya viongozi uchaguzi huitishwa tena na kujazwa nafasi iliyo achwa wazi labda kwa sababu ya kushindwa uongozi au kuhama.

Viongozi
Katika parokia viongozi wa kamati tendaji ya parokia wanao utaratibu wa kukutanan maramoja kwa mwezi

Parokia inaandaa semina za viongozi wake kikanda na kiparokia , mfano katika kipindi cha mwaka 2017 kumekuwa na semina kwa kamati tendaji na halmashauri ya walei parokia, semina mbili zilifanyika zinazohusu uongozi

Huduma zitolewazo
Huduma zitolewazo ni pamoja na huduma za kuombea wagonjwa inayotolewa na paroko na paroko msaidizi

Pia ipo kamati ya afya ya parokia ambayo huusika moja kwa moja katika kuwatembelea wahitaji katika jumuiya na familia na kuwapa mahitaji mbali mbali

Paroko na paroko msaidizi wamekuwa pia na muda ambao wameupanga wa kuzitembelea familia zenye migogoro mbalimbali

Halmashauri ya walei parokia inaundwa na viongozi wa kamati tendaji ya kanda na wenyeviti wa vyama na vikundi vya kitume ngazi ya parokia

Mawasiliano
Njia kuu za mawasiliano ni matangazo ya kila dominika, simu, barua pepe yaani E mail ,

Kamati
Katika paarokia zipo kamati za kikatiba na zisizo za kikatiba, kamati zisizo za kikatiba ni kama zifuatazo
    -kamati ya uhamasishaji wa sherehe
    -kamati ya ulinzi
    -Kamati ya afya
    -kamaati ya ardhi na ukarabati majengo

Kamati zote hizi zina umuhimu kiparokia, na haziingiliani kimajukumu isipokua pale ambapo itaonekana kuna umuhimu wa kushirikiana.

Malengo
Kuwaimarisha wakatoliki na wasio wakatoliki kumjua kristo na Mungu kwa kukua kiimani hasa kuishi kwa sakramenti takatifu yaani Ubatizo , Komunio , Kipaimara, Ndoa na miito mitakatifu ya utawa na upadre.
Moja ya malengo mengine ya parokia ni kuifanya parokia iweze kujitegeme kwa kupitia vitega uchumi kama kumbi na miradi mingine itakayoonekana inafaa kwa sasa na nyakati zijazo baala ya kutegeme sadaka na michango kutoka kwa wa umini

Vyama na vikundi

Parokia ina vyama vya kitume vipatavyo 13,

Vyama na vikundi vipo chini ya kamati tendaji.

Taarifa za fedha na vyama vya vikundi hutolewa kila mwisho wa mwaka, na baada ya miaka mitatu hufanywa uchaguzi.

Ushiriki  katika vyama vya kitume na dekania na jimbo  ni mzuri na upo ushirikishwaji.


Fedha
Katika parokia mpango wa fedha unao tumika ni ule wa jimbo

Mapato na matumizi ya fedha yanajulikana kwa waumini, na yanatolewa mara nne kwa  mwaka na kusomwa katika mkutano wa halmashauri ya walei parokia

Matoleo ya kila dominika husomwa kwa waumini dominika inayofuata

Michango ya jimbo inatolewa kwa utaratibu kama ambavyo maelekezo yanavyo takiwa

Changamoto

  • Fedha hazipelekwi banki kwa wakati na hivyo kujikuta zinafanyiwa matumizi mengine
  • Utoaji wa zaka kama amri ya kanisa ni hafifu na wa kusuasua
  • Mapadri na watawa  bado wanaonekana kuwa hawatoshi kutokana na mahitaji

Ulinzi na usalama
Ulinzi na usalama parokiani ni wa kuridhishisha kwa kushirikiana na kamati husika

Miradi
Hakuna  mradi unaoendeshwa na parokia

Wanaafunzi ambao wanasoma seminari kutoka parokia ya maurusi ni Wawili tu mpaka kufikia 2017, na mtawa yuko mmoja kutoka shirika la masister wa usambara

Kihistoria
Hakuna mabadiliko yeyote ya kihistoria.

JE UNATAFUTA

PAROKIA?

Upate majibu yako haraka zaidi
Ramani ya Parokia
Hakuna ramani kwa sasa...
Kuhusu Kanisa Katoliki

Ofisi ya Halmashauri ya Walei Jimbo Kuu la Dar es salaam inapatikana makao makuu ya Jimbo,
Kanisa la St. Joseph, barabara ya Sokoine na Manseld street.

P.O Box 167, Dar es Salaam, Tanzania
Tel: +255 762 024 199
Email: mawasiliano@waleijimbodaresalaam.org
            darwaleijimbo@yahoo.com
Web: www.waleijimbodaresalaam.org

Kwa Habari kemkem za Kanisa jiunge nasi

Andika email yako hapo juu, na upokee taarifa za H/walei

Copyright © 2025. All Rights reserved by H/Walei Jimbo Kuu la Dar es salaam