PAROKIA YA MIKOCHENI


PAROKIA Y MTAKATIFU MARTHA MIKOCHENI
Parokia ya mt Matha ilizaliwa 2006

Parokia hii inapatikana mikocheni  katika dekania  ya Mt petro

Idadi ya waumini ni kati ya 1275, na idadi hii imepatikana kutokana na sense iliyofanyika kutokana na taarifa zilizo patikana katika JNNk za mwaka 2016. Sensa nyingine imefanyika tayari 2017 kwa kila jumuiya kuleta idadi ya waumini wake kutoka katika kila jumuiya.

Parokia haina kigango kwa sasa.

Katika parokia zipo jumuiya ndogo ndogo 21 ingawa jumuiya moja inasali na kushiriki katika Parokia ya Mt petro.

Jumuiya zinatumia majina ya watakatifu.

Kwa kila jumuiya kuna wastani wa kaya 12-15.

Katika parokia kuna kanda 4, na kanda hizo ziimegawanyika kutokana na mahali zilipo, na kila kanda ina wastani wa JNNK 5, na uongozi wa kanda unapatikana kwa kupitia uchaguzi uliofanywa na viongozi wa jumuiya zake, na kanda zote zina uongozi uliokamilika. Majina ya kanda hayafuati majina ya watakatifu

JNNK na kanda/Mitaa inasali pamoja siku za juimatano jioni lakini nyingi ni siku za jumamosi (asubuhi)

Mahudhuriakwa ujumla katika jumuiya na kanda yanaridhisha na yana rekodiwa katika rejista ya kila jumuiya.

Ushiriki wa wanaume  ni wakusuasua, Viongozi wanachukua hatua ya kuongea nao na kuwahamasisha ili waweze kuhudhria ipasavyo

Jumuiya zinazoonyesha kuwa na changamoto zinatembelewa ili kutatua changamoto zao.

Katika parokia ya Mt Matha, JNNK hua zinaaadhimisha misa za aina mbili
•    Kubariki nyumba kila mwaka baada ya pasaka
•    Kufanyika misa za somo wa jumuiya

Uongozi katika JNNK, Kanda, Mitaa na vigango umekamilika.

Pale inapoonekana kuwepo na upungufu wa kiongozi mmojawapo chaguzi za kuziba nafasi zilizoachwa wazi hufanywa.

Uongozi wa halmashauri hukutana kila baada ya miezi mitatu.

Huduma za kiroho zinazotolewa ni pamoja na ;

Kutembelea wagonjwa hospitalini, Wafungwa ,na kuwahudumia wahitaji

Ziko changamoto nyingi katika kuzihudumia JNNK ambazo ni pamoja na hizi zifuatazo;

Baadhi ya nyumba zinakuwa mbali na zingine

Badhi ya wanajumuiya hawashiriki shughuli za kanisa lakini wanataka kupata huduma.

Baadhi ya waumini kuhama na kwenda maeneo mengine.

UONGOZI
Kamati tendaji ipo na imekamilika kikatiba

Kamati tendaji hukutana mara moja kwa mwezi na muda wa kikao ni wastani wa saa limoja tokea kuanza kwa kikao, na baba paroko ni mmoja wa wajumbe wa kikao.

Halmashauri ya walei ya parokia inaundwa na viongozi watano kutoka katika kila kanda , kamati tendaji ,wenye viti wote wa vyama vya kitume ngazi ya parokia na jumla ya wajumbe ni 29. Kukutana ni mara mbili kwa mwaka au Zaidi, na kama kunadharura vikao hufanyika siku ya dominika

Agenda na riport za vikao vinapatikana kwa wakati na vinatunzwa

Ofisi Walmashauri ya Walei ya parokia imejikamilisha kuweza kufanya shughuli zake bila wasiwasi.

Njia za mawasiliano zinazo tumika ni kama vile;
I.    Barua pepe E mail
II.    Simu
III.    Kupitia matangazo siku za dominika.

KAMATI
Zipo kamati ndogo ndogo za kikatiba ambazo wajumbe wake wametokana na kamati tendaji ya parokia

Kamaati nyingine ni zile zisizo za kikatiba yaani;

Kamati ya Ulinzi, Kamati ya Afya, Kamati ya ujenzi na kamati ya usafi. hizi kamati zinasaidiana katika utekelezaji wa shughuli za parokia lakini hazina muingiliano.

Kamati ndogo ndogo zinaleta taarifa kwa kamati tendaji kila baada ya miezi mitatu

Kuna kalenda ambayo inaeleza matukio ya mwaka kiparokia na dekania, ambazo kimsingi imeandaliwa kwa kushirikiana na waumini ili kupata taarifa mbalimbali

Njia zinazo tumika katika kuwaarifu waumini mipango ya parokia ni kwa njia ya matangazo yanayosomwa siku za dominika pamoja na matangazo yanayoweka katika mabao ya matangazo.

VYAMA, MASHIRIKA NA JUMUIYA ZA KITUME
Vyama mashirika na jumuiya za kitume viko 8.
a.    WAWATA,
b.    UWAKA,
c.    VIWAWA,
d.    SHIKWAKA,
e.    Karismatiki katoliki
f.    Legio Maria
g.    Moyo mt wa yesu

Vyama hivi vina wanachama wachache na baadhi yake havina kabisa.

Vyama na vikundi vya kitume vinafanya kazi kulingana na katiba ya halmashauri ya walei japo bado ni wachanga.

Vyama hivi havina ofisi lakini baadhi yao wanavifaa tu vya kazi za kiofisi

VMJ havitoa taarifa pamoja na repoti ya fedha kwa uongozi wa parokia

Ushirikiano na ushiriki wa VMJ na parokia katika shughuli za kidekania na jimbo uko vizuri.

SEMINA MBALIMBALI KATIKA UENDELEVU WA IMANI, UONGOZI NA UTEGEMEZAJI
Hakuna semina na mafungo yanayoandaliwa kiparokia kwa sasa katika JNNK na kanda.

Uongozi wa parokia na, kamati tendaji na halmashauri ya walei ya parokia hawajapatiwa semina bado

Kwa upande wa semina za kiroho na tegemeza kanisa bado hazijafanyika pia

Hali ya Imani katoliki kwa ujumla katika parokia inaridhisha.

Halikadhalika swala la utoaji kwa waumini lina ridhisha kwa kiasi chake

Pia utoaji wa zaka kama amri ya kanisa unaridhisha.

Parokia inatoa michango kamili ya jimbo kama inavyo paswa na kwa wakati.

FEDHA NA MIPANGO
Mpango wa fedha unaotumika ni ule wa jimbo

Mapato na matumizi ya parokia yanajulikana kwa waumini, Taarifa ya mapato na matumizi ya kila wiki zinatolewa  kila dominika na majumuisho ya mwaka mzima yanatolewa kwa halmashauri ya walei ya parokia na kusomwa kwa waumini pamoja na bajeti ya parokia kwa mwaka unaofuata.

Matoleo ya kila dominika yanatangazwa kwa waumini kila dominika inayofuata

Fedha yote inapelekwa benki kwa wakati

ULINZI NA USALAMA
Hali ya ulinzi na usalama kwa ujumla iko vizuri,na walinzi wanotumika wanatoka katika kampuni binafsi

MAENDELEO YA KIUCHUMI
Hakuna miradi yoyote kwa sasa, lakini katika swala la maendeleo ya parokia kuna ujenzi wa ukumbi wa parokia lakini baada ya hapo utaanza ujenzi wa grotto ya bikira Maria

MAMBO YA JUMLA
Katika swala la mipaka , kuna mgogoro kati ya parokia ya mt petro na parokia ya mt Matha

Idadi ya mapadre / watawa waliopo kwa sasa inatosheleza hii ni kutokana na idadi ya waumini waliopo kwa sasa

JE UNATAFUTA

PAROKIA?

Upate majibu yako haraka zaidi
Ramani ya Parokia
Hakuna ramani kwa sasa...
Kuhusu Kanisa Katoliki

Ofisi ya Halmashauri ya Walei Jimbo Kuu la Dar es salaam inapatikana makao makuu ya Jimbo,
Kanisa la St. Joseph, barabara ya Sokoine na Manseld street.

P.O Box 167, Dar es Salaam, Tanzania
Tel: +255 762 024 199
Email: mawasiliano@waleijimbodaresalaam.org
            darwaleijimbo@yahoo.com
Web: www.waleijimbodaresalaam.org

Kwa Habari kemkem za Kanisa jiunge nasi

Andika email yako hapo juu, na upokee taarifa za H/walei

Copyright © 2025. All Rights reserved by H/Walei Jimbo Kuu la Dar es salaam