Habari
Tarehe : 08 February, 2019

HALMASHAURI YA WALEI

UCHANGIAJI WA MFUKO WA UINJILISHAJI

kutokana na kuwepo kwa mahitaji makubwa ya uendeshaji shughuli za Halmashauri Walei Jimbo Kuu la Dar es salaam, imeonekana kuwepo haja ya kuongeza kipato kupitia vyanzio mbalimbali katika shughuli za uinjilishaji, Hivyo yamepitishwa maazimio mbalimbali ya namna ya kupata fedha kwaajili ya kutunisha mfuko. imeonekana michango ya Pentekoste pekee haitoshi kukidhi mahitaji ya shughuli za kila siku za Halmashauri Walei jimbo. 

Kutokana na mahitaji hayo;

1. kila Parokia , Kuanzia Mwaka ujao, yaani 2022 Januari zitachangia shilingi 200,000

2. Kila kiongozi wa Halmashauri Walei Jimbo kuu la Dar es salaam atachangia shilingi 100,000. Fedha hizi zitatolewa kwa kwa mwaka mzima.

3. Pia , zimeandaliwa bahasha ambazo wamesambaziwa Baadhi ya wadau ambao watachangia ili kutunisha mfuko wa Uinjilishaji.

4.Pia imebuniwa miradi mbalimbali huko Kisarawe ya ufugaji ngombe wa nyama, Mbuzi na ufugaji wa nyuki

Kwa mpango huo basi Imefunguliwa Akaunti maalumu kwaajili ya kuchangia Mfuko wa uinjilishaji ijulikanayo kwa jina la UINJILISHAJI WALEI DSM, Akaunti namba ni; 00211515091101

Pia Kuna lipa kwa M- Pesa namba 5040013, Jina UINJILISHAJI HALMASHAURI WALEI JIMBO.

Kaulimbiu ya Kisinodi Inasema (Ushirika, Ushiriki na Umisionari), Sisi ndio wamisionari wa Leo. Walei ndio Nguzo ya Kanisa, na Kanisa litajengwa na sisi wenyewe.

Mungu awabariki sana.


 


Document Attachment :
Halmashauri ya Walei 19-Jan-2019 08-50-52 0 Kb


Kuhusu Kanisa Katoliki

Ofisi ya Halmashauri ya Walei Jimbo Kuu la Dar es salaam inapatikana makao makuu ya Jimbo,
Kanisa la St. Joseph, barabara ya Sokoine na Manseld street.

P.O Box 167, Dar es Salaam, Tanzania
Tel: +255 762 024 199
Email: mawasiliano@waleijimbodaresalaam.org
            darwaleijimbo@yahoo.com
Web: www.waleijimbodaresalaam.org

Kwa Habari kemkem za Kanisa jiunge nasi

Andika email yako hapo juu, na upokee taarifa za H/walei

Copyright © 2025. All Rights reserved by H/Walei Jimbo Kuu la Dar es salaam