Changamoto

Changamoto

Zipo changamoto nyingi katika uendeshaji shughuli mbali mbali ukizingatia jimbo ndio muhimili mkubwa katika kusimamia,kuratibu malengo na maazimio mpaka ngazi ya chini kabisa, hivyo zipo changamoto nyingi kama vile;
•    Upungufu wa mapadre baaada ya kuongezeka vituo vya sala,Vigango na Parokia
•    Baadhi ya waumini kutangatanga katika madhehebu na makanisa mengine.
•    Vijana wengi kukosa moyo wa kujiunga na upandre /utawa
•    Mmomonyoko wa maadili kuongezeka
•    Madhehebu na vikanisa vidogo vidogo kuchipua
•    Uharibifu wa Imani kutokana na utandawazi
•    Maudhhurio hafifu katika shughuli mbalimbali za kikanisa mfano; Ibada na JNNK kwa akina Baba na Vijana
•    Vijana wengi kuishi uchumba sugu au suria
•    Nyota ya kijani na athari katika uzazi

NINI KIFANYIKE
•    Kusisitiza mafundisho ya sakramenti (Biblia na Katekisimu endelevu) pamoja na mafuundisho mengine ya kiroho ili kujenga Imani ya waumini.
•    Mapadre/Watawa kuishi maadili yao na kuacha kupenda malimwengu
•    Kusisitiza mafundisho ya ndoa ya mara kwa mara ili kujenga ufahamu Zaidi katika maisha ya kimahusiano ya ndoa
•    Mafundisho yatolewe juu ya matumizi sahihi ya utandawazi pamoja na athari zake katika jamii.
•    Kuhimiza vijana kujiunga na utawa/Utawa.



Kuhusu Kanisa Katoliki

Ofisi ya Halmashauri ya Walei Jimbo Kuu la Dar es salaam inapatikana makao makuu ya Jimbo,
Kanisa la St. Joseph, barabara ya Sokoine na Manseld street.

P.O Box 167, Dar es Salaam, Tanzania
Tel: +255 762 024 199
Email: mawasiliano@waleijimbodaresalaam.org
            darwaleijimbo@yahoo.com
Web: www.waleijimbodaresalaam.org

Kwa Habari kemkem za Kanisa jiunge nasi

Andika email yako hapo juu, na upokee taarifa za H/walei

Copyright © 2025. All Rights reserved by H/Walei Jimbo Kuu la Dar es salaam